RADAR JNIA KUANZA KAZI DECEMBER 21




Kutoka: Gazeti la Jamvi la Habari
BAADA ya kukamilika ujenzi wa jengo la kufunga mfumo wa rada ya kisasa wa  kuongoza ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataif wa Julius  Nyerere (JNIA), hatimaye mashine zimeanza kufungwa.
Ufungwaji wa rada hiyo, nimipango ya serikari ya awamu ya tano ambapo mradi huo, utahusisha viwanja vingine vitatu ambvyo ni Uwanja wa Kimataifa Kilimanjaro (KIA), Songwe na Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mhandisi Mshauri wa Miradi JNIA, Stephine Mwakasasa, alisema kazi hiyo inatarajiwa kukamilika Desemba 21 mwaka huu.
Alisema, mara baada ya kufungwa mfumo huo, utaanza kazi  kwa majaribio, hata hivyo, alibainisha kuwa Mkurugenzi Mkuu Hamza Johari ndiyo atatangaza rasmi siku ya ufunguzi wa mfumo huo na kuanza kazi.
“Kama mnavyoona kwamba kazi inaendelea vizuri tu, tunatarajia kumaliza kazi hii muda mfupi lakini kwa kuhusu kufunguliwa rasmi hilo watalizungumzia Watendaji wa TCAA,”alisema Mwakasasa.
Mwakasasa, alisema kukamilika kwa mfumo huo warada ya kisasa kutsidia kuongeza kampuni za ndenge kuja kutua katika uwanja huo kitendo ambacho kitaliongezea taifa mapato.
Naye Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATAA), Aristid Kanje, alisema chuo hicho kimezalisha wataalam wa kitanzania 7235 tangu kilipoanzishwa miaka 35 iliyopita.
Chuo hicho kilianzishwa mara baada ya kuvujika Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 tukio ambalo lilifanya Tanzania isiwe na chuo cha kufundishia wataalamu wake wa sekta ya Usafiri wa Anga.
Kanje, alisema kuanzishwa chuo hicho kumelisaidia taifa kupunguza gharama za kupeleka wataalamu wake kwenda kusoma nje ukilinganisha na awali wakati watanzia walipokuwa wakienda vyuo vya nje.
Alisema, miongoni mwa wahitimu hao, wanaume ni 6214 na wanawake 1021, ambao hivi sasa wameweza kulisadidia taifa katika kuleta mabdiliko ya kiutendaji katika sekta hiyo.
“Chuo lilianzishwa mwaka 1985 na hiyo ni baada ya ya kuvunjika Jumuiya ya Afrika Masharik mwaka 1977 kutokana mazingira hayo Tanzania ilibaki ikiwa haina chuo cha kufundishia wataalamu wake,”alisema Kanje.
Kanje, alisema chuo hicho kinatoa mafunzo kwa kiwango cha Kimataifa ambapo hivi sas kinadahili hata wageni ambao wanahudhuria mafunzo katika chuo hicho.
Aidha,Kanje alisema ili kuimarish ufafanisi katika chuo hicho,Serikali imenunua mtambo wa kisasa kwa ajili ya kufundishia, wenye thamani ya zaidi  Sh. Bili 1.
Pia alisema hivi sasa chuo hicho kina mpango wa kujenga chuo kikubwa cha kimataifa, ambapo uongozi uko katia mchakato wa hatua za mwisho kukamilisha adhima yake hiyo hususani kupata eneo maalum.
Kaimu Mkurugezi wa Ufundi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mbila Mdemu, alisema, serikali iliamua kuunda vyombo tendaji/Wakala mbalimbali zitakazokuwa zikitekeleza majukumu kwa uhuru lakini chini ya uangalizi wa karibu wa serikali.

MWANAMKE AUAWA NA TEMBO

 

 


Chris Bomola

Tembo hao ni wa kutoka hifadhi ya Lwafi

Mwanamke wa miaka 60, ameuawa na tembo katika Wilaya ya Kalambo iliyoko Magharibi mwa Tanzania.
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema, tukio hilo lilitokea wakati marehemu akiwa anarejea kutoka shambani kwake majira ya saa nne asubuhi.
Hifadhi ya Lwafi inapatikana pembezoni mwa barabara ya kutoka Tanzania kuelekea Zambia.
Akithibitisha kutokea tukio hilo Mkuiu wa Wilaya ya kalambo Bi Julieth Binyura amewataka wananchi kuacha kuwafukuza tembo wanapoingia katika maeneo hayo badala yake kusubiri wataalamu kufanya kazi hiyo.

RAMAPHOSA: HAKUNA KINGA YA RAISI ZUMA DHIDI YA MASHITAKA YANAYOMKABILI



Raisi wa Chama cha ANC Cyril Ramaphosa ameiambia Kamati Kuu ya Chama hicho kuwa  Hakuna kinga dhidi ya mashitaka yanayomkabili Raisi wa nchi ya Afrika Kusini Bwana Jackob Zuma.Na sio moja ya makubaliano katika kukabidhiana madaraka.
Chanzo: News24

KUTANA NA HARMONY MDOLI WA NGONO ANAYEONGEA



Mageuzi ya teknolojia yamesababisha mabadiliko mbalimbali katika njia za binadamu, Kwa siku za karibuni kumekua na ongezeko kubwa la uzalishaji wa Midoli ya ngono, ambayo inasemekana mahitaji yake kwa sasa yameongezeka.
Harmony ni moja ya zao la mageuzi ya midoli ya ngono, mdoli Harmony anaweza kuongea na kutembea kwa kutumia teknolojia ya robot iliyotumika kumtengeneza.

SERIKALI KUJENGA ''FLYOVER'' NYINGINE SABA



Serikali katika kukabiliana na tatizo la foleni za barabarani imepanga kujenga vivuko saba vya juu vya barabara (flyover)
hayo yamesemwa na Msemaji wa Serikali Dr Hassan Abbas wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Barabara zitakazohusika na ujenzi wa flyover hizo ni Chang'ombe, Uhasibu, Kamata, Morocco, Mwenge, Magomeni na Tabata.

WAKILI WA UPINZANI KENYA ATIMULIWA



Wizara ya mambo ya ndani nchini Kenya imesema wakili wa upande wa upinzani Miguna Miguna alipata hati ya kusafiria ya Kenya kinyume cha sheria na hivyo kutimuliwa kwake kwenda nchini Canada hakukukiuka sheria za nchi wala haki zake
Jana usiku mamlaka nchini Kenya zilimfukuza ghafla Miguna na kumpandisha katika ndege ya shirika la Uholanzi la KLM kuelekea nchini Canada. Hatua hiyo ilizua mjadala mkubwa huku wengi wakiilaani serikali ya Kenya kuwa ilikiuka sheria za uhamiaji za nchi hiyo na haki za kiraia za bwana Miguna
Katika taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya Kenya msemaji wa wizara hiyo Mwenda Njoka amesema bwana Miguna "kwa makusudi alishindwa" kuweka wazi kuwa alikuwa na uraia wan chi nyingine wakati alipopatiwa hati ya kusafiria ya Kenya mnamo Machi 2009.
"Kwa mantiki hiyo hati ya kusafiria ya Kenya ya bwana Miguna ilikuwa na bado ni batili", alifafanua bwana Njoka
Miguna alifukuzwa nchini Kenya mara baada ya kushiriki katika kiapo kisicho rasmi cha Raila Odinga kuwa rais wa watu wa Kenya mwezi uliopita.
CHANZO: BBC SWAHILI

Kategori

Kategori