RADAR JNIA KUANZA KAZI DECEMBER 21




Kutoka: Gazeti la Jamvi la Habari
BAADA ya kukamilika ujenzi wa jengo la kufunga mfumo wa rada ya kisasa wa  kuongoza ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataif wa Julius  Nyerere (JNIA), hatimaye mashine zimeanza kufungwa.
Ufungwaji wa rada hiyo, nimipango ya serikari ya awamu ya tano ambapo mradi huo, utahusisha viwanja vingine vitatu ambvyo ni Uwanja wa Kimataifa Kilimanjaro (KIA), Songwe na Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mhandisi Mshauri wa Miradi JNIA, Stephine Mwakasasa, alisema kazi hiyo inatarajiwa kukamilika Desemba 21 mwaka huu.
Alisema, mara baada ya kufungwa mfumo huo, utaanza kazi  kwa majaribio, hata hivyo, alibainisha kuwa Mkurugenzi Mkuu Hamza Johari ndiyo atatangaza rasmi siku ya ufunguzi wa mfumo huo na kuanza kazi.
“Kama mnavyoona kwamba kazi inaendelea vizuri tu, tunatarajia kumaliza kazi hii muda mfupi lakini kwa kuhusu kufunguliwa rasmi hilo watalizungumzia Watendaji wa TCAA,”alisema Mwakasasa.
Mwakasasa, alisema kukamilika kwa mfumo huo warada ya kisasa kutsidia kuongeza kampuni za ndenge kuja kutua katika uwanja huo kitendo ambacho kitaliongezea taifa mapato.
Naye Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATAA), Aristid Kanje, alisema chuo hicho kimezalisha wataalam wa kitanzania 7235 tangu kilipoanzishwa miaka 35 iliyopita.
Chuo hicho kilianzishwa mara baada ya kuvujika Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 tukio ambalo lilifanya Tanzania isiwe na chuo cha kufundishia wataalamu wake wa sekta ya Usafiri wa Anga.
Kanje, alisema kuanzishwa chuo hicho kumelisaidia taifa kupunguza gharama za kupeleka wataalamu wake kwenda kusoma nje ukilinganisha na awali wakati watanzia walipokuwa wakienda vyuo vya nje.
Alisema, miongoni mwa wahitimu hao, wanaume ni 6214 na wanawake 1021, ambao hivi sasa wameweza kulisadidia taifa katika kuleta mabdiliko ya kiutendaji katika sekta hiyo.
“Chuo lilianzishwa mwaka 1985 na hiyo ni baada ya ya kuvunjika Jumuiya ya Afrika Masharik mwaka 1977 kutokana mazingira hayo Tanzania ilibaki ikiwa haina chuo cha kufundishia wataalamu wake,”alisema Kanje.
Kanje, alisema chuo hicho kinatoa mafunzo kwa kiwango cha Kimataifa ambapo hivi sas kinadahili hata wageni ambao wanahudhuria mafunzo katika chuo hicho.
Aidha,Kanje alisema ili kuimarish ufafanisi katika chuo hicho,Serikali imenunua mtambo wa kisasa kwa ajili ya kufundishia, wenye thamani ya zaidi  Sh. Bili 1.
Pia alisema hivi sasa chuo hicho kina mpango wa kujenga chuo kikubwa cha kimataifa, ambapo uongozi uko katia mchakato wa hatua za mwisho kukamilisha adhima yake hiyo hususani kupata eneo maalum.
Kaimu Mkurugezi wa Ufundi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Mbila Mdemu, alisema, serikali iliamua kuunda vyombo tendaji/Wakala mbalimbali zitakazokuwa zikitekeleza majukumu kwa uhuru lakini chini ya uangalizi wa karibu wa serikali.

MWANAMKE AUAWA NA TEMBO

 

 


Chris Bomola

Tembo hao ni wa kutoka hifadhi ya Lwafi

Mwanamke wa miaka 60, ameuawa na tembo katika Wilaya ya Kalambo iliyoko Magharibi mwa Tanzania.
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema, tukio hilo lilitokea wakati marehemu akiwa anarejea kutoka shambani kwake majira ya saa nne asubuhi.
Hifadhi ya Lwafi inapatikana pembezoni mwa barabara ya kutoka Tanzania kuelekea Zambia.
Akithibitisha kutokea tukio hilo Mkuiu wa Wilaya ya kalambo Bi Julieth Binyura amewataka wananchi kuacha kuwafukuza tembo wanapoingia katika maeneo hayo badala yake kusubiri wataalamu kufanya kazi hiyo.

RAMAPHOSA: HAKUNA KINGA YA RAISI ZUMA DHIDI YA MASHITAKA YANAYOMKABILI



Raisi wa Chama cha ANC Cyril Ramaphosa ameiambia Kamati Kuu ya Chama hicho kuwa  Hakuna kinga dhidi ya mashitaka yanayomkabili Raisi wa nchi ya Afrika Kusini Bwana Jackob Zuma.Na sio moja ya makubaliano katika kukabidhiana madaraka.
Chanzo: News24

KUTANA NA HARMONY MDOLI WA NGONO ANAYEONGEA



Mageuzi ya teknolojia yamesababisha mabadiliko mbalimbali katika njia za binadamu, Kwa siku za karibuni kumekua na ongezeko kubwa la uzalishaji wa Midoli ya ngono, ambayo inasemekana mahitaji yake kwa sasa yameongezeka.
Harmony ni moja ya zao la mageuzi ya midoli ya ngono, mdoli Harmony anaweza kuongea na kutembea kwa kutumia teknolojia ya robot iliyotumika kumtengeneza.

SERIKALI KUJENGA ''FLYOVER'' NYINGINE SABA



Serikali katika kukabiliana na tatizo la foleni za barabarani imepanga kujenga vivuko saba vya juu vya barabara (flyover)
hayo yamesemwa na Msemaji wa Serikali Dr Hassan Abbas wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Barabara zitakazohusika na ujenzi wa flyover hizo ni Chang'ombe, Uhasibu, Kamata, Morocco, Mwenge, Magomeni na Tabata.

WAKILI WA UPINZANI KENYA ATIMULIWA



Wizara ya mambo ya ndani nchini Kenya imesema wakili wa upande wa upinzani Miguna Miguna alipata hati ya kusafiria ya Kenya kinyume cha sheria na hivyo kutimuliwa kwake kwenda nchini Canada hakukukiuka sheria za nchi wala haki zake
Jana usiku mamlaka nchini Kenya zilimfukuza ghafla Miguna na kumpandisha katika ndege ya shirika la Uholanzi la KLM kuelekea nchini Canada. Hatua hiyo ilizua mjadala mkubwa huku wengi wakiilaani serikali ya Kenya kuwa ilikiuka sheria za uhamiaji za nchi hiyo na haki za kiraia za bwana Miguna
Katika taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya Kenya msemaji wa wizara hiyo Mwenda Njoka amesema bwana Miguna "kwa makusudi alishindwa" kuweka wazi kuwa alikuwa na uraia wan chi nyingine wakati alipopatiwa hati ya kusafiria ya Kenya mnamo Machi 2009.
"Kwa mantiki hiyo hati ya kusafiria ya Kenya ya bwana Miguna ilikuwa na bado ni batili", alifafanua bwana Njoka
Miguna alifukuzwa nchini Kenya mara baada ya kushiriki katika kiapo kisicho rasmi cha Raila Odinga kuwa rais wa watu wa Kenya mwezi uliopita.
CHANZO: BBC SWAHILI

KAMPUNI YA MUGABE YAKABILIWA NA MASHTAKA


Kampuni moja ya rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe inatakiwa kuondoka katika kipade kimoja cha ardhi kinachomilikiwa na shule moja la sivyo ishtakiwe.
Kampuni hiyo kwa Jina Gushungu Holdings inadaiwa kunyakuwa kipande hicho cha ardhi chenye ukubwa wa hekari 23 katika eneo moja la makaazi ya mji wa Harare.
Kanisa la Reform linasema kuwa ardhi hiyo inamilikiwa na kundi la shule zake la Eaglesvale.
Wakili wa shule hiyo Rodney Makausi aliambia BBC kwamba mwaka 2016 serikali ilichukua ardhi hiyo kwa nguvu.
Serikali baadaye ikaondoa madai yake baada ya swala hilo kuwasilishwa mahakamani.
HABARI: BBC SWAHILI

Kigwangwala atembelea nyumba ya Baba wa Taifa-Magomeni

Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Hamis Kingwangwala amefanya ziara ya kutembelea nyumba ya Rais wa Kwanza na Baba wa Taifa Julius Nyerere, iliyopo magomeni jijini Dar es salaam. 
Picha kwa hisani ya Hamis Kingwagwala (twitter page) 

Rais Trump avishutumu vyombo vya Habari kwa kuandika habari Feki

Rais Donald Trump azungumza katika mkutano ulioandaliwa na World Economic Forum huku akivituhumu kuandika habari za uongo na kupotosha hotuba zake. 
Picture: Reuters

Kagame azungumza na Donald Trump

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Taifa la Marekani Donald Trump, ambapo wawili hao pamoja na mambo mbalimbali wamezungumzia mahusiano mazuri kati ya Marekani na mataifa ya Africa. 


Viongozi hao walikutana mjini Davos nchini Switzerland walipokuwa wamehudhuria mkutano ulioandaliwa na World Economic Forum. 

Tido Mhando Aburuzwa mahakamani

Mkurugenzi wa zamani TBC afikishwa mahakamani na kushitakiwa kwa makosa ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia hasara serikali.
Picha: citizen online

Dawa za nguvu za kiume zawaponza Zambia

Kiongozi wa mkoa, Chanda Kasolo, ameiambia BBC kuwa mara baada ya kunywa dawa hizo, walianza kutapika kitu ambacho kilisababishwa na mchanganyiko wa chakula, pombe na dawa hizo za asili.

''Baada ya majibu ya vipimo kupatikana , inaonekana kuwa mchanganyiko wa pombe, vyakula na dawa hiyo, ulisababisha mchafuko wa mfumo wa chakula na hivyo ikahusishwa na kipindupindu lakini baada ya kuwauliza maswali, baadaye walikiri kuwa walikunywa dawa ya kuongeza nguvu katika tendo la ndoa''

Wagonjwa hao bado wapo katika kituo hiko cha kipindupindu na wanaendelea vizuri na matibabu, aliongeza bwana Kasolo.

Wanaume hao watatu wanatoka katika mji mdogo wa katete, na si wagonjwa wa kipindupindu bali walikunywa dawa ya kuongeza nguvu ya kufanya tendo la ndoa inayojulikana kama Mvubwe.

Ugonjwa wa kipindupindu uliolipuka mwaka jana ulisababisha vifo vya watu takribani 70, kusini mwa Afrika.

Rais Edgar Lungu mwezi uliopita, alitoa agizo kwa jeshi la Zambia kusafisha maeneo ya masoko na kuondoa uchafu ambao ndio saabu ya kipindupindu.


Habari Mali ya BBC Swahili

Croatia yatoa kitabu cha hadithi cha watoto,kinachoonyesha wazazi wenye jinsia moja

Chanzo: BBC Swahili. 


Kwa mara ya kwanza Croatia, kitabu cha watoto cha hadithi za kusimulia kitandani Kimejumuisha wahusika ambao ni wapenzi wa jinsia moja. kinajumuisha msichana aliye na baba wawili, na mvulana aliye na mama wawili. Je, unadhani kitabu kama hicho kinafaa watoto? #GNBSwahili

GNBSwahili

Kategori

Kategori