SIMBA MTANI JEMBE WA UKWELI

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,
Akiuwahi mpira wa uliokuwa umetemwa na golikipa wa Yanga SC, Deogratius Munish ‘ Dida’ ambaye alishindwa ‘ kiki ya umbali wa mita zipatazo 23’ ( adhabu ndogo) iliyokuwa imepigwa na mchezaji aliyekuwa bora zaidi katika mchezo huo baina ya mahasimu wa kandanda nchini, Yanga SC na Simba SC uliofanyika katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Emmanuel Okwi ambaye alivaa beji ya unahodha kwa mara ya kwanza kwa upande wa Simba alipiga mpira ambao ulitemwa na Deo kisha kiungo, Awadh Juma akafunga bao la kuonga kwa timu yake katika dakika ya 30.
Dakika tatu kabla ya muda wa mapumziko mshambulizi Elius Maguli akafunga bao lingine akimalizika mpira uliokuwa unarudi uwanjani baada ya kugonga mwamba kufuatia ‘ kiki’ ya kiungo, Mganda, Simon Sserunkuma. Mabao hayo mawili yalisimama hadi mwisho wa mchezo na kwa mara ya pili mfululizo ‘ Wekundu wa Msimbazi’ wanatwaa ushindi wa ‘ Nani Mtani Jembe-2’. Ikumbukwe kuwa mwaka uliopita, Yanga ilipoteza kwa mabao 3-1.
MARCIO MAXIMO…….
Wakati Fulani katika kipindi cha pili kocha huyo wa Yanga alionekana ‘ akijaribu kufunga na mchezaji wake’. Nilimshangaa zaidi pale alipojaribu ‘ kuhitaji huduma ya mchezaji alikwisha choka’. Maximo alikuwa ni mwenye presha kubwa na alitamani walau kuona timu yake ikifunga bao dhidi ya Simba lakini hakuwa na mbinu bora.
Patrick Phiri amecheza mchezo wa 12 dhidi ya Yanga akiwa kocha wa Simba, amepoteza mara moja tu na kwenda sare mara tano, ushindi mara sita bila shaka ‘ unaweza kumuita kiboko ya makocha wa Yanga’, ilikuwa ngumu kwa Yanga kushinda kutokana na mfumo mgumu wa kiuchezaji walioingia nao, pia uchaguzi wa wachezaji haukuwa bora.
Mbuyu Twite, Emerson Oliveira, Haruna Niyonzima, Saimon Msuva na Andrey Coutinho walianza katika eneo la kiungo wakiwa wachezaji watano ambao mbele yao alisimama mshambulizi, Kpah Sherman. Yanga walianza vizuri mchezo huo, walicheza kwa kupasiana huku wakiwa na hali ya kujiamini. Wingi wa wachezaji wao katika eneo la kiungo kulifanya waonekane ni timu imara zaidi, lakini hali hiyo ilitoweka baada ya Simba kuanza kuwabana na kucheza pia kwa kujiamini.
Tukio la Kelvi Yondan la kumfanyia madhambi Emmanuel Okwi katika dakika 15 liliongeza presha kwa Yanga, inawezekana mwamuzi ‘ Mwanamama’ Jonesia Rukyaa alichemsha kutokana na kutofuatilia kwa makini tukio hilo la Kelvin kumchezea faulo Okwi pasipo kuwa na mpira. Wachezaji wa Yanga wakiongozwa na Niyonzima mara kwa mara walikuwa wakimzonga mwamuzi. Awadh, Jonas Mkude na Sserunkuma wakaanza kutawala kiungo, na nguvu ile na stamina walizokuwa nazo wachezaji wa Yanga katika robo saa ya kwanza ya mchezo zikatoweka. Mawasiliano kati ya safu ya kiungo na ile ya mshambulizi ‘ yakafa’, wakakubali kusogezwa nyuma ya lango lao na Simba wakamaliza mechi kwa stahili ya ‘ rebound’ mipira iliyorudi kutoka katika goli la Yanga.
Katika muda wa dakika 90, Maximo alitumia washambualiaji wanne, Sherman aliyeanza kama mshambulizi huru, kabla ya Danny Mrwanda kuingia dakika ya 46 kuchukua nafasi ya Coutinho ambaye hakufanya lolote katika mfumo wa awali wa 5-4-1. Alipoingia Mrwanda angalau hata Maximo mwenyewe aliona dalili za kupata bao lakini alikwisha chelewa, Phiri alimmaliza na wachezaji waliouchezesha ‘ sawia’ mfumo wa 4-3-3.
Kwa mara ya pili, Yanga chini ya Maximo imeshindwa kupata goli dhidi ya Simba, lakini baada ya suluhu-tasa, mwezi Oktoba katika mchezo wa ligi kuu, Phiri alishajua namna ya kuishinda Yanga. Ni kuwawkea mshambulizi msumbufu na mwenye nguvu walinzi ‘ wenye jabza’ Nadir Haroub na Kelvin.
Maguli alikuwa bize kukimbia na mipira, haijalishi mara ngapi aliicha nyuma, lakini kila aliposogea katika eneo la hatari la Yanga alikuwa mwenywe nguvu. Tuwe wa kweli, Yanga inahitaji mlinzi wa Kimataifa labda ndiyo wataweza kushindana barani Afrika hapo mwakani.
Kelvin anahitaji kujitazama upya, amekuwa ni mchezaji mwenye hasira za haraka huku matukio yake yakiwa ya wazi. Alikimbizwa hasa na alionekana kuchoshwa na washambuaji watatu wa Simba waliokuwa wakihamahama, nawazungumzia Okwi, Maguli na Ramadhani Singano. Kitu cha kujivunia kwa Yanga ni uwepo wa kiongozi wa kweli, nahodha, Nadir, Kelvin anaweza kujifuna mengi kutoka wa ‘ patna wake huyo’ ili kuifanya Yanga kuwa bora.
max
Maximo alianza na wachezaji wote wa kigeni, lakini chaguo la kuwaazisha nje, Dilunga, Ngassa na Mrwanda na kuwaanzisha, Coutinho, Sherman ambaye alitua nchini siku mbili kabla ya mchezo huo hakika halikuwa chaguo bora na amevuna alichopanda.
Sserunkuma alicheza kwa mara ya kwanza, aliipandisha timu kwa kasi mara nyingi hasa baada ya Simba kutawala mchezo, alikimbia na mipira huku akigawa pasi zilizofika kwa walengwa, juhudu zake zilizaa bao la pili kwa timu yake baada ya kusogea na mpira na kupiga kiki ya umbali iliyogonga mwamba na kumkuta mfungaji katika dakika ya 42.
Mganda huyo anayeichezea Express alicheza kwa dakika 84 na kumpisha Shaaban Kisiga anaisaidia sana Simba ambao wanahaha kupata kiungo mwenye kupandisha timu kwa kasi huku akipiga pasi za uhakika. Alimpunguzia majuku mengi Mkude, na alitawala ‘ duara’ akishirikiana na Awadh. Nahodha, Joseph Owino alianzia katika benchi kumpisha, Mganda, Juuko Murushid kucheza na chipukizi, Hassan Isihaka.
Nassoro Chollo alianza katika nafasi ya ulinzi wa kulia alipoteza mipira mingi huku akipiga pasi za hovyo mara kadhaa, alicheza dakika zote 90 lakini bado anahitaji kujiimarisha zaidi na kupunguza papara anapokuwa na mpira. Mohhammed Hussein aliendelea kuwa na kiwango bora, alianza katika beki tatu na aliimarisha ukuta wa Simba.
SIMBA SC, IVO Mapunda, Nassoro CHOLL, Mohamed Hussein ‘ TSHABALALA’/ Issa Rashid ‘ BABA UBAYA’ dk 66, Hassan ISIHAKA, Juuko MURUSHID/ Joseph OWINO dk 47, Jonas MKUDE, Ramadhani SINGANO/ Said NDEMLA dk 74, AWADH Juma, Elius MAGULI/ Danny SSERUNKUMA dk 84, Simon SSERUNKUMA/ Shaaban KISIGA dk 84, Emmanuel OKWI.
YANGA SC, Deogratius MUNISH, Juma ABDUL/ Hussein JAVU dk 79, Oscar JOSHUA, Nadir HAROUB, Kelvin YONDAN, MBUTU Twite/ Hassan DILUNGA dk 39, EMERSON Oliveira/ Salum TELELA dk 55, Haruna NIYONZIMA, Kpah SHERMAN/ Mrisho NGASSA dk 63, Saimon MSUVA, Andrey COUTINHO/ Danny Mrwanda dk 46…
0714 08 43 08
habari kwa hisani ya Shaffii Dauda Blog




WANAZUONI WATOA TAMKO WAPINGA MAAZIMIO YA PAC,WAMTAKA RAIS APUUZE MAAZIMIO YA PAC

WAKATI Ikulu ikitoa taarifa na kusema kuwa Rais Jakaya Kikwete atafanya maamuzi juu ya sakata la akaunti ya ESCROW kuhusiana na maazimio ya bunge, jumuiya ya wanazuoni wameibuka na kuponda maazimio ya Bunge yaliyotokana na Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC).

Pia, jumuiya hiyo imesema ipo mbioni kuanzisha hati ya maombi maalumu kwa Rais Kikwete (Petition Form) itakayosainiwa na mamilioni ya watanzania kumuomba Rais apuuze maazimio hayo ya bunge.

Akizungumza jana na waandishi wa habari, kwa niaba ya jumuiya hiyo, Kaimu Mratibu wa jumuiya hiyo, Shaibu Sufiani alisema wameamua kufanya hivyo ili kuungana dhidi ya mabepari na madalali wa rasilimali za nchi.
Alisema jumuiya hiyo inaundwa na vijana wasomi wa vyuo vikuu nchini na nje ya nchi, ambapo amedai wana wajibu chanya kuhakikisha Tanzania inaendeshwa kwa kufuata misingi imara ya ukweli, uwazi, uwajibikaji.

“Tunapaswa kuzingatia msingi mkuu wa haki kwa kila mtu na watanzania waelewe kuwa kujiuzuru sio ushujaa au uzalendo. Jiulize wote waliojiudhuru hadi sasa ni wazalendo wa kweli wa nchi yetu?,’’alisema Sufiani.
Sufiani alisema panapotokea masuala yote ya kitaifa, masuala yanayohusu kuwajibishana, kutuhumiana, kushughulikiana kama wengine wanavyosema, basi lazima misingi yote iende sambamba na haki kwa kila mtuhumiwa.

Kwa mujibu wa Kaimu Mratibu huyo, alisema sote tunakumbuka kwamba Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amekabidhi ripoti ya uchunguzi kuhusiana na sakata la TEGETA ESCROW.

Alisema msingi mkuu wa sakata hilo, unahusiana na kampuni ya kufua umeme ya IPTL, ambapo CAG kwenye uchunguzi wake iliarifu juu ya hadidu za rejea zaidi ya 11 iliyopewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Bunge na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini.

“Kwa nyakati tofauti, na kwa namna tofauti, sisi wenyewe, tumeshuhudia ripoti hiyo, na tumestahajabishwa na kugeuzwageuzwa kwa mapendekezo ya ripoti hiyo kulikofanywa na kamati ya bunge ya PAC,’’alisema.

Sufiani alisema ripoti ya CAG pamoja na viambatanisho vyake vyote, tumesoma na kuvirudia mara kwa mara hakuna sehemu, ambayo mkaguzi ameshauri, ama kupendekeza, ama kutafsiri kwamba pesa iliyokuwepo katika akaunti hiyo ni mali ya UMMA.

Pia, alisema katika ripoti ya CAG, hakuna sehemu hata moja au kurasa iliyosema kwamba Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amelisababishia hasara Taifa au Waziri au Katibu wa Nishati na Madini.

“Ripoti ya CAG hakuna sehemu yoyote inayosema kwamba fedha iliyotolewa kwenye akaunti ya ESCROW ni ama bilioni 321 au bilioni 306 kama wanavyouaminisha umma. Tunatambua mtachelewa kutuelewa, na mtashangaa kwa nini tumeamua kusema haya, lakini ni lazima tubadili sasa mfumo wetu wa siasa za Tanzania na siasa za kutatua matatizo na changamoto kama ilivyo sasa,’’alisema.

Sufiani alisema wanasiasa hasa wabunge, wamekuwa wakifanya maamuzi kishabiki, kichuki, kimaslahi binafsi na bila kuzingatia ukweli na misingi ya utawala bora huku ripoti ya CAG ikisema wazi imefanya jitihada stahili kuhakikisha taratibu zinafuatwa ili kujiondoa kwenye madhara yanayoweza kutokea baada ya fedha kutoka.

“Ripoti ya CAG haijamtia hatiani mtu yeyote. Tunashindwa kuelewa misingi ya Kamati ya PAC ya kutaka kuwajibishwa kwa watu bila ya kuwa na hatia.
vyovyote itakavyokuwa, na vyovyote itakavyotafsiriwa, imetoka wapi?,’’alisema.

Sufiani alisema kuwapoteza watu kama Waziri wa Pro.MUHONGO, kwenye utumishi wa umma, kwa sababu tu Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo hana mahusiano mazuri na madalali wa rasilimali za nchi hii, ambao historia imeonyesha maeneo kadhaa walipoiaminiwa na kuharibu.

Alisema pia, kumpoteza Profesa Muhongo kwa sababu tu tangu kuingia kwake ofisini ameziba mianya ya uchotwaji mkubwa wa fedha za watanzania kupitia sekta ya madini, na sasa mabepari wameungana na wabunge wenye husuda kupambana dhidi ya ukweli na haki anayosimamia Waziri.

“Kumpoteza Muhongo kwa sababu tu yeye na Katibu mkuu wake Eliakim Maswi, hawana mawasiliano mazuri na baadhi ya wabunge au wajumbe wa PAC juu ya kitendo chao kudhibiti udalali wa rasilimali,’’alisema

Sufiani alisema watanzania wanapaswa kujiuliza maswali, ambayo PAC wanapaswa kutujibu ikiwemo kutueleza, ni katika ukurasa wa ngapi, aya ya ngapi, nukta ya ngapi iliyopo kwenye ripoti ya CAG inayosema kwamba ESCROW ni MALI YA UMMA?.

Pia, alisema wanaitaka PAC iwaeleze, ni katika ukurusa wa ngapi, iliyopo kwenye ripoti ya CAG inayosema kwamba watendaji hao wa serikali wamefanya makosa na wanapaswa kuwajibisha.

“Tunaitaka PAC itueleze, kama kulikuwa na mchezo mchafu, na wakauthibitisha, iweje Wizara ya Fedha isihusike?, kwa nini Gavana wa BOT na timu yake na Waziri wa Fedha na timu yake nao wasihusike kwenye hilo kwa kuwa fedha ilikuwa kwao,” alisema.

Alisema kama kweli kulikuwa na mchezo mchafu, iweje BRELLA, na Wizara inayoisimamia ambayo ni viwanda na biashara na Waziri wake na timu nzima wasiwajibishwe nao kusajili kampuni ambayo wanadai siyo halali.

“Kama ni kweli kuna tatizo, iweje TRA wakubali kupokea kodi ya zaidi ya bilioni 30 kutoka kwa mbia wa IPTL ambao ni VIP iliyotokana na mauzo ya hisa 30% kwa PAP?. Kwa nini TRA isiwajibishwe kwa kupokea fedha haramu na kuziingiza kwenye mapato ya serikali ilihali ikijua ni fedha haramu?,”alisema.

Kutokana na hali hiyo, Sufiani alisema suala nzima la ESCROW limegubikwa na siasa, maslahi binafsi, chuki, wivu na kukomeshana, Hivyo tunamuomba Rais Kikwete  asitekeleze azimio hata moja mpaka kwanza umma utakapoelewa ukweli halisi wa mbivu na mbichi na kila lililo nyuma ya pazia kuhusiana na sakata hilo.

“Tunamuomba Rais aunde chombo huru, ili suala hili lichunguzwe na kufanyiwa maamuzi huru ikiwemo na tuhuma za baadhi ya Wabunge kuhongwa, kununuliwa na kuwa mawakala wa Benki ya Standard Charterd,’’alisema.

Hivyo, alisema wanamuomba Rais, aviagize vyombo vyake vya ulinzi na usalama viwachunguze wabunge wote wanohusika kwa tuhuma kutumiwa, kuhongwa na kununuliwa ili kutuondolea watetezi wetu wa rasilimali.











SOURCE GAZETI LA MAJIRA, HABARI LEO.
NAFASI ZA KAZI TCU PITIA HAPA

NAFASI ZA KAZI TCU PITIA HAPA

Tanzania Commission for Universities (TCU) POSITION DESCRIPTION:

From The Guardian


Report to: Director of Finance and Administration

Job Summary

Human Resources Officer will provide quality human resource support
to all directors and staff in the Tanzania Commission for Universities
Collect, analyze, tabulate and maintain personnel data and statistics;
Assist in the administration of recruitment and staff allocation; welfare;
Deals wi1h general disciplinary matters for junior staff;
Oversees the general cleanliness of office premises;
Preparation of manpower development plans, training and career development programmes;
Ensure that staff houses, office buildings and other estates are maintained;
Looks after the welfare of employees in matters related to administration, medical treatment, housing and transport. Ensures that all estates, fixed assets and other property are properly insured;
Assist in identifying manpower needs and proper utilization of human resources;
Ensures that machinery and other office equipment are well maintained;
Any other duties as may be assigned by the relevant executive.


Academic Qualifications

The ideal candidate for this position should have the following qualifications and
experience.
Possession of a University degree with specialization or bias in either Public
Administration, Human Resources Management and Business Administration or equivalent qualification with minimum experience of not less than three years in the field of Human Resources Management, ",

Personal Attributes
In additional to the above skills and qualifications the applicant for the above
position is required to have the following attributes:
A very high level of integrity, honesty and sense of responsibility;
Ability to work in a dynamic team;
Ability to produce expected results
Ability to self manage and meet deadlines
Willingness to work beyond the call of duty
Computer literacy is necessary
Must not be above 35 years of age

Remuneration
Successful candidate will be paid according to Tanzania Commission for
Universities salary scale




APPLICATION INSTRUCTIONS:

MODE OF APPLICATION
1. Applicants who meet the stated requirements for the advertised post and would like to serve the Tanzanian Public Service through Tanzania Commission for Universities, should send their applications to:

The Executive Secretary Tanzania Commission for Universities
P.O. Box 6562
DAR E S SALAAM

2. Signed application letters must be accompanied by:
(a) Proof of Tanzanian citizenship (affidavits will not be accepted)
(b) Applicant's current CV and two passport size photographs in colour. (c) Photocopies of academic and professional certificates
(d) Names and fulll contact addresses and daytime telephone numbers of
three referees.
3. All application must be posted; personal delivery will not be entertained.
4. All applications must be in hand writing.
5. Applications should reach the Tanzania Commission for Universities latest by the close of business on 19th December 2014.
6. The title of the position applied for should be marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
7. Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action.
8. Applicants for senior positions currently employed in the public service should route their application letters through their respective employers.

NOTE: Only short-listed candidates who meet the above criteria will be contacted and those who will not hear from us should consider themselves
unsuccessful.


Legal Officer II POSITION DESCRIPTION:

From The Guardian

Report to: Deputy Executive Secretary
Academic Qualifications
Holder of LLB Degree and has successfully completed one year internship with not less than three years experience in legal matters. Skills in computer applications will be an added advantage.

Main Duties and Responsibilities

Indexing, filing and registered government / Commission notices and all other legal documents
Dealing with legal routine matters and correspondence addressed to or involving the Commission.
Advising and helping Higher Learning Institutions on the design and refinement of their charters / constitutions gazetting of institutions with Commission charters / constitutions.
Drafting prescribed Commission legal documents and forms;
Filling and appearing for criminal and civil proceedings in court on behalf of the Commission.
Assisting in the interpretation of laws, government circulars, directives and other matters
Performs any other duties allocated to him / her by superior.

Personal Attributes
In additional to the above skills and qualifications applicant for the above position are required to have the following attributes:
A very high level of integrity, honesty and sense of responsibility;
Ability to work in a dynamic team;
Ability to produce expected results
Ability to self manage and meet deadlines, and
Willingness to work beyond the call of duty
Computer literacy is necessary
Must not be below 30 years of age

Remuneration
Successful candidate will be paid according to Tanzania Commission for
Universities salary scale





APPLICATION INSTRUCTIONS:

MODE OF APPLICATION
1. Applicants who meet the stated requirements for the advertised post and would like to serve the Tanzanian Public Service through Tanzania Commission for Universities, should send their applications to:

The Executive Secretary Tanzania Commission for Universities
P.O. Box 6562
DAR E S SALAAM

2. Signed application letters must be accompanied by:
(a) Proof of Tanzanian citizenship (affidavits will not be accepted)
(b) Applicant's current CV and two passport size photographs in colour. (c) Photocopies of academic and professional certificates
(d) Names and fulll contact addresses and daytime telephone numbers of
three referees.
3. All application must be posted; personal delivery will not be entertained.
4. All applications must be in hand writing.
5. Applications should reach the Tanzania Commission for Universities latest by the close of business on 19th December 2014.
6. The title of the position applied for should be marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
7. Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action.
8. Applicants for senior positions currently employed in the public service should route their application letters through their respective employers.

NOTE: Only short-listed candidates who meet the above criteria will be contacted and those who will not hear from us should consider themselves
unsuccessful.


Internal Auditor II POSITION DESCRIPTION:

From The Guardian

Report to: Chief Internal Auditor

Main duties and responsibilities
Checking of salary records
Checking of banking reconciliation
Audit invoices and local purchases
Auditing of journal entries
Auditing of receipts and payments vouchers
Any other duties assigned by the Chief Internal Auditor

Academic Qualification and Experience
The ideal candidate for this position should have the following qualifications and experience.
Holders of B.Com or BBA degree majoring in Accountancy or equivalent qualifications with possession of Certified Public Accountant (Tanzania) (CPA) ( (T), Association of Certified Chartered Accountants (ACCA), Chartered Accountant (CA), with not less than three years experience in areas of auditing issues. Computer skills are essential.

Personal Attributes
( In additional to the above skills and qualifications the applicant for the above position is required to have the following attributes:
A very high level of integrity, honesty and sense of responsibility;
Ability to work in a dynamic team; ,
Ability to produce expected results
Ability to self manage and meet deadlines
Willingness to work beyond the call of duty
Computer literacy is necessary
Must not be below 30 years of age
Successful candidate will be paid according to Tanzania Commission for
Universities salary scale



APPLICATION INSTRUCTIONS:

MODE OF APPLICATION
1. Applicants who meet the stated requirements for the advertised post and would like to serve the Tanzanian Public Service through Tanzania Commission for Universities, should send their applications to:

The Executive Secretary Tanzania Commission for Universities
P.O. Box 6562
DAR E S SALAAM

2. Signed application letters must be accompanied by:
(a) Proof of Tanzanian citizenship (affidavits will not be accepted)
(b) Applicant's current CV and two passport size photographs in colour. (c) Photocopies of academic and professional certificates
(d) Names and fulll contact addresses and daytime telephone numbers of
three referees.
3. All application must be posted; personal delivery will not be entertained.
4. All applications must be in hand writing.
5. Applications should reach the Tanzania Commission for Universities latest by the close of business on 19th December 2014.
6. The title of the position applied for should be marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
7. Presentation of forged academic certificates and other information in the CV will necessitate to legal action.
8. Applicants for senior positions currently employed in the public service should route their application letters through their respective employers.

NOTE: Only short-listed candidates who meet the above criteria will be contacted and those who will not hear from us should consider themselves
unsuccessful.

Mafanikio ya Professor Muhongo Yaliza Watanzania Wengi



 professor Muhongo (Waziri Nishati na Madini)

UTEKELEZAJI wa shinikizo la kuvuliwa madaraka
kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo, linaloendelea kutolewa na
wabunge na baadhi ya wanasiasa kwa Rais
Jakaya Kikwete, huenda ukaacha masononeko
kwa wananchi walionufaika na kipindi kifupi cha
uongozi wa waziri huyo.
Profesa Muhongo aliyejitengenezea uadui kwa
wafanyabiashara na wanasiasa, kutokana na
misimamo yake ya kulinda maslahi ya umma na
kuzungumza ukweli, huku akijiamini
kulikotafsiriwa kuwa ni dharau, hatima ya uongozi
wake ipo mikononi mwa Rais Kikwete, ambaye
ameshauriwa na Bunge kutengua uteuzi wake.
Katika azimio la saba, kati ya maazimio manane
ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
lililomalizika mwishoni mwa mwezi uliopita,
kuhusu utoaji wa fedha katika akauti ya Tegeta
Escrow, iliyokuwa katika Benki Kuu ya Tanzania
(BoT), mamlaka ya uteuzi wa Profesa Muhongo,
imeshauriwa kutengua uteuzi huo.

Bunge linashauri na kuazimia Waziri wa Nishati
na Madini, Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Mwanasheria Mkuu, Katibu
Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,
wawajibishwe na mamlaka ya uteuzi itengue
uteuzi wao, limeeleza azimio hilo la saba.
Usambazaji umeme
Kama Rais Kikwete atatekeleza ushauri huo wa
Bunge na shinikizo la wanasiasa na
wafanyabiashara, uongozi wa muda mfupi wa
Profesa Muhongo takribani miaka miwili,
utakumbukwa kwa umahiri wa kusambaza
umeme vijijini.
Kabla ya kuteuliwa kwa Profesa Muhongo,
Watanzania asilimia 14 tu ndio waliokuwa
wakitumia nishati ya umeme, kati yao asilimia 12
walikuwa watumiaji wa mijini na asilimia mbili tu,
ndio walikuwa watumiaji wa vijijini.
Kwa mujibu wa takwimu za Serikali, kati ya
mwaka 2007 na mwaka 2010, kulikuwa na
ongezeko la asilimia nne tu la watumiaji wa
umeme, hali iliyoonesha kuwa ongezeko la
Watanzania waliokuwa wakipata umeme, lilikuwa
asilimia moja kwa mwaka.
Lakini baada ya kuteuliwa kwa Profesa Muhongo
katika nafasi hiyo, katika muda mfupi wa uongozi
wake, idadi ya Watanzania wanaotumia umeme
iliongezeka na kufikia asilimia 36 katikati ya
mwaka huu.

Kwa hatua hiyo, uongozi wa Profesa Muhongo
ulivuka malengo ya Ilani ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM), ambayo ndio msingi wa
utekelezaji wa malengo ya Serikali, iliyotaka
Serikali kuhakikisha ifikapo mwaka 2015, asilimia
30 ya Watanzania wawe wanapata umeme.
Baada ya kupita malengo ya Ilani ya Uchaguzi ya
CCM, Profesa Muhongo aliamua kuweka malengo
mapya, ambapo alitarajia ifikapo 2015, asilimia
45 mpaka 50 ya Watanzania wawe na fursa ya
kutumia umeme.

Miongoni mwa Watanzania wanaokiri hilo ni
Diwani wa Kata ya Manga wilayani Tarime,
Omolo Ochola ambaye pia ni mchimbaji mdogo
wa madini kutoka Rorya.
Ochola alipozungumza na gazeti hili wiki hii,
alisema Waziri Muhongo amefanya kazi kubwa,
amesambaza umeme vijiji vingi hapa nchini na
kudhibiti ubadhirifu uliokuwepo hapo awali.
Mbali na Ochola, Mbunge wa Ntera, Livingston
Lusinde (CCM), alisema yeye hawezi kuona aibu
kuzungumzia mafanikio ya uongozi wa Profesa
Muhongo, huku akitoa mfano wa Tanesco kupigia
simu wateja ili ikawaunganishie umeme, kuwa
haikuwahi kutokea kabla ya uongozi wake.
Bei ya uunganishaji
Katika kutimiza malengo hayo, uongozi wa
Profesa Muhongo, ulitangaza punguzo la
gharama za kuunganisha umeme majumbani
kutoka Sh 177,000 za awali hadi Sh 27,000
vijijini.
Awali, punguzo hilo lilitolewa kwa mikoa ya Lindi
na Mtwara, ambako bomba la kusafirisha gesi
kwenda Dar es Salaam limeanzia na limepita,
lakini baada ya muda gharama hizo zilishushwa
kwa vijiji vyote nchi nzima.
Profesa Muhongo mwenyewe alisema gharama
hizo zitahusu miradi inayosimamiwa na Wakala
wa Umeme Vijijini (REA), katika kipindi ambacho
wakandarasi watakuwa wakiendelea na awamu
ya pili ya miradi iiliyoanza Machi mwaka huu na
kutarajiwa kukamilika kati kati ya mwakani.
Profesa Muhongo alisema kuwa katika awamu ya
kwanza ya miradi iliyomalizika Desemba mwaka
jana, wanavijiji walilipa gharama kubwa, hivyo
uongozi wake uliamua kupunguza malipo hayo, ili
huduma hiyo ya nishati iwafikie watu wengi
zaidi.
Kufuta mgawo
Kuhusu suala la mgawo wa umeme, Profesa
Muhongo mwaka 2012 alisema mgao wa umeme
hautakuwepo tena na haukubaliki kamwe.
Profesa Muhongo alisema hadi Juni 2012 uwezo
wa mitambo ya kufua umeme (installed
capacity) ulikua megawati 1,375.74 (gesi asilia
ikiwa ni asilimia 40, maji asilimia 41 na mafuta
asilimia 19).

Alifafanua kuwa uwezo huo, ulikuwa ni ongezeko
la megawati 367 sawa na asilimia 36
ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74
uliokuwepo Juni, 2011.
Alisema mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka
2011/12 yalifikia wastani wa MW 820.35
ikilinganishwa na MW 730 kwa mwaka 2010/11.
Tangu wakati huo, hakujatokea mgawo mkali wa
umeme kama uliotokea mwanzoni mwa mwaka
2011, na miaka ya nyuma ya hapo.

Tanzania kabla ya uongozi wa Profesa Muhongo,
ilikuwa ikikabiliwa na mgawo wa umeme wa
mara kwa mara, ambao mbali na kuathiri maisha
ya watu wa kawaida kutokana na kusababisha
mfumko wa bei, pia uliathiri sekta ya viwanda
ambapo baadhi vilitishia kufunga.
Kutokana na mgawo wa mara kwa mara,
mwanzoni mwa mwaka 2011, Shirikisho la Wenye
Viwanda Tanzania (CTI), liliwahi kutoa taarifa ya
kutishia kufungwa kwa viwanda 50 kati ya 280,
huku vingine vikitishia kupunguza uzalishaji,
kutokana na makali ya mgawo wa umeme.
Wamiliki hao walidai kupitia CTI kwamba, hawana
uwezo wa kutumia jenereta kwa ajili ya shughuli
za uzalishaji viwandani, kwa vile umeme wa
jenereta utawalazimu kulipia gharama za
matumizi ya nishati hiyo maradufu, tofauti na ile
inayozalishwa na Shirika la Umeme (Tanesco).
Walitoa mfano kuwa wakitumia umeme wa
Tanesco kwa kila kilowati moja, wanalipia senti
za dola ya Marekani nane mpaka tisa, lakini
wakitumia umeme wa jenereta, kwa kila kilowati
moja, wanatumia senti za dola ya Marekani 18
mpaka 20.
Mbali na hao, CTI ilieleza pia kuwa asilimia 15 ya
wanachama walitishia kuongeza bei ya kuuzia
bidhaa wanazozalisha na athari yake kwa
mapana, ilielezwa kuwa viwanda vitakosa
mapato, ajira kwa watumishi wa viwandani
zitapotea na Serikali pia itakosa mapato
yanayotokana na kodi za viwanda.
Aidha Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), ilieleza
kuwa mfumko wa bei ulipanda na kufikia asilimia
6.4 kutoka asilimia 5.6, sababu kubwa ikiwa ni
mgawo wa umeme.

Ofisi hiyo ilitoa mfano wa bei ya vyakula na
vinywaji baridi, kwamba ilipanda kutoka asilimia
2.9 na kufikia asilimia 6.7 kutokana na mgawo
wa umeme.
Kushusha bei ya umeme Baada ya kufanikiwa
kufuta mgao wa umeme, kusambaza umeme kwa
wananchi na kuunganisha umeme kwa wananchi
kwa gharama nafuu, mwanzoni mwa mwaka huu,
Profesa Muhongo, alitangaza kusudio lake la
kushusha bei ya umeme.
Diwani Ochola wa Manga wilayani Tarime,
alisema Profesa Muhongo alikuwa amejiandaa
kushusha zaidi gharama za umeme mwakani.
Naye Musa Onyango, mchimbaji mdogo kutoka
Rorya, alisema gharama za umeme zilikuwa
zikipanda kila mwaka na kuwakatisha tama
Watanzania ikilinganishwa na kipindi cha mwaka
mmoja wa Profesa Muhongo ambapo kumekuwa
na ahueni kubwa ikilinganishwa na wakati wa
viongozi waliotangulia Kusudio hilo la kushusha
bei, lilitarajiwa kuanza kuonekana mara bomba la
gesi kufika jijini Dar es Salaam na mitambo ya
umeme kuanza kutumia gesi badala ya mafuta
mazito.

Uongozi wa Profesa Muhongo, uliweka wazi kuwa
wafanyabiashara wanaouzia umeme Tanesco,
wanauza uniti moja kwa kati ya Dola ya Marekani
senti 33 na 50.
Bei hiyo ya umeme kwa Tanesco kwa mujibu wa
takwimu za Serikali, ni kubwa kuliko bei ya
umeme ambayo shirika hilo linauza kwa
Watanzania wanaotumia umeme mdogo wa
majumbani, umeme wa kati kwa
wafanyabiashara, umeme wa kati wa viwandani
na umeme mkubwa kwa viwanda vikubwa, na
kubwa kuliko bei ya umeme ya mashirika ya
umeme ya nchi za Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa Takwimu za Tanesco, wateja wa
majumbani, uniti moja ya umeme wanauziwa kwa
dola ya Marekani senti 19, wateja wa biashara
senti 13 na viwanda vya kati na vikubwa senti
10.

Umeme wa taa za barabarani ni senti 19, wakati
Tanesco inanunua kwa senti 33 na 50. Profesa
Muhongo alisema bei ya umeme iliyopo, ni kwa
muda tu na itashuka sana bomba la gesi
likikamilika, kwa sababu hata mitambo ya kufua
umeme inayotumia mafuta nayo, itatumia gesi na
mitambo mipya ya gesi italetwa.
Alisema Serikali inataka umeme mwingi utokane
na gesi, jua, upepo na joto ardhi, lakini wapo
wanaokataa bomba lisije Dar es Salaam na
nyuma yao, wapo wafanyabiashara ambao
wanahofia kuwa mwisho wa biashara yao ya
kuuzia Tanesco umeme kwa bei ya juu umefika.
Msimamo huo wa Profesa Muhongo, uliwahi
kuungwa mkono na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
aliyesema mwishoni mwa Januari mwaka huu
alipokuwa Mtwara, kuwa Serikali imedhamiria
kuachana na umeme huo wa mafuta na kama
wafanyabiashara hao watataka kuendelea na
biashara hiyo, ni vyema wabadilishe mitambo yao
iwe ya gesi na sio ya mafuta kama ilivyo sasa
hivi.

Wataalamu wa gesi
Kutokana na ugunduzi mkubwa wa gesi
uliofanyika nchini, Profesa Muhongo pia
alianzisha utaratibu wa kusomesha Watanzania
wengi zaidi katika vyuo vya nje ya nchi katika
masuala ya gesi na mafuta, ili wananchi
wasimamie rasilimali hiyo kwa manufaa ya taifa
lao na vizazi vyao.
Lengo la Profesa Muhongo katika hilo, ni
kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya kwanza
yenye wataalamu wengi wa mafuta na gesi,
katika nchi za bara la Afrika, baada ya miaka
mitano ijayo kwa kuwa na wataalamu zaidi ya
300 watakaokuwa wamesomea masuala hayo nje
ya nchi.
Pia amefanya juhudi kushawishi watanzania
ambao ni wataalamu mafuta na gesi zaidi ya 10
wanaofanya kazi nje ya nchi hususani nchini
Canada na Uingereza, mpaka wakakubali kurejea
kufanya kazi hizo nchini.

Utata wa kumwajibisha
Hatua ya Bunge kutaka Profesa Muhongo
awajibishwe, imetokana na maoni ya Mwenyekiti
wa Bunge wa Kamati ya Fedha za Serikali (PAC),
Kabwe Zitto, kuwa fedha hizo Sh bilioni 321 ni za
umma na utoaji wake na kwamba hatua ya
kulipwa kwa kampuni ya Independent Power
Tanzania Limited (IPTL), iligubikwa na harufu ya
ufisadi.
Hata hivyo, Profesa Muhongo katika utetezi
wake, alisema wakati wa kufunga akaunti hiyo
kulikuwa na Sh bilioni 182.77 tu, wakati deni
baada ya kupiga hesabu, lilikuwa Sh bilioni
275.20 na zote ni fedha za IPTL, zilizotokana na
mauzo ya umeme wake katika Shirika la Umeme
(Tanesco), na hivyo bado kampuni hiyo inaidai
shirika hilo la umeme Sh bilioni 123.90.
Mbali na kueleza kuwa kampuni hiyo ya IPTL
bado inaidai Tanesco, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, Frederick Werema, ambaye naye
anatakiwa kuondolewa, alisisitiza kuwa akaunti
ya Escrow haikatwi kodi, ila kodi hiyo hukatwa
kwa mpokeaji wa fedha hizo na kutaka Mamlaka
ya Mapato (TRA), kwenda kudai kodi yake kwa
IPTL.
Profesa Muhongo na Werema mpaka sasa
msimamo wao ni kwamba fedha hizo si za
umma, huku Profesa Muhongo akisisitiza kuwa
mbali na kuwa si za umma, pia Serikali bado
inadaiwa Sh bilioni 123.90.
Lakini hata taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali (CAG), hajathibitisha kuwa
fedha hizo ni za umma, bali ilieleza kuwa kuna
uwezekano kuwa katika fedha hizo, kuna fedha
za Tanesco, fedha za Serikali kwa maana ya
kodi na fedha za IPTL, ambazo ni mauzo ya
umeme kwa Tanesco.

Habari kwa Hisani ya Habari Leo.

SHAHIDI: SIAJONA BALENGA AKIMUUZIA NYUMBA MACHA.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana ilisikiliza ushahidi wa mfanyabiashara maarufu wa Dar es Salaam, Hans Aingaya Macha akitoa ushahidi katika kesi inayomkabili ya kughushi.
Macha alitoa ushahidi wake, wakati upande wa mshitakiwa unaoongozwa na Wakili Deogratius Ringia mbele ya Hakimu Devotha Kisoka mahakama hapo jana.
Mfanyabiashara huyo, alidai mahakamani hapo kuwa nyumba ya ghorofa tano kilichopo katika kiwanja namba 183 ‘A’ kilichopo Kigogo, aliinunua kwa Ramadhan Balenga huku akiwa pia anamdai Balenga.
Hata hivyo, Wakili wa serikali Nassoro Katuga alipomuuliza swali mshitakiwa huyo aonyeshe ushahidi wake, ikiwemo nyaraka za madeni na awataje majina ya mashahidi waliokuwepo wakati akinunua nyumba hiyo ya ghorofa tano kwa sh. Milioni 20, alidai wapo.
Kitendo ambacho, kilimfanya mshitakiwa huyo kudai mahakamani hapo kwa jina moja tu, ndipo aliwapowaambia awataje na yeye aliwataja akiwemo mfanyakazi wa Balega aitwaye Mohammed Waziri.
Alipomaliza kutoa ushahidi wake, Macha, ndipo zamu ya Wazir ilifika, ambaye alidai mahakamani hapo kuwa hakuwahi kushuhudia mauzo yeyote yakifanyika kwa kuwa wakati huo alishaondolewa katika biashara alizokuwa akizifanya.
“Sifahamu chochote kuhusiana na Balenga kuuza nyumba, ingawa niliambiwa na watu wa pembeni, akiwemo Macha mwenyewe, hivyo huo ndio ukweli wenyewe Mheshimiwa Hakimu ninaoujia,’’kauli ambayo iliamsha cheko katika chumba cha mahakama kutokana na ushahidi wake huo.
Katika hatua nyingine, aliyekuwa mke wa Balenga, Nully Ahmady alidai mahakamani hapo kuwa hata yeye hakushuhudia wakati akiuza nyumba hiyo, kwa kuwa alikuwa tayari ameshaachana naye. Kesi hiyo inaendelea tena mahakamani hapo.

 Picha: Mfanyabiashara Macha

SOURCE: Jamii Forums.

Kategori

Kategori