Mwanamume mmoja nchini Kenya ameshtakiwa kusambaza picha alizodai ni za wanajeshi wa Kenya waliouawa nchini Somalia akitumia WhatsApp.


Eddy Reuben Illah ameshtakiwa kwa kueneza: “Picha zinazodaiwa kuwa za miili ya maafisa wa Majeshi ya Ulinzi ya Kenya (KDF), waliodaiwa kushambuliwa na kuuawa eneo la El-Adde nchini Somalia ukijua kwamba ni za uchochezi na zingesababisha hofu na wasiwasi miongoni mwa raia.”
Anadaiwa kusambaza picha hizo kwenye kundi la watumiaji wa WhatsApp kwa jina A young peoples union (Muungano wa vijana).
Bw Illah amekanusha mashtaka hayo mbele ya hakimu mwandamizi wa Kiambu, mji ulio karibu na Nairobi, Bw Justus Mutuku.
Juhudi za wakili wake Bw Edwin Sifuna kutaka aachiliwe huru kwa dhamana huru zimegonga mwamba na akatakiwa kuweka dhamana ya Sh100,000 na mdhamini wa Sh50,000, gazeti la Daily Nation limeripoti.
Kesi hiyo itatajwa Februari 2 na kuanza kusikilizwa Februari 12.
SOURCE: BBC SWAHILI
PICHA: BBC SWAHILI


EmoticonEmoticon